Conte amtaka Mourinho kuwacha kuzungumzia Chelsea - HABARI TANZANIA

Post Top Ad

Thursday, 19 October 2017

demo-image

Conte amtaka Mourinho kuwacha kuzungumzia Chelsea

Responsive Ads Here
_98376914_c4f8d685-745b-444a-a728-1a9efa99b5b0
Image captionConte amtaka Mourinho kuwacha kuzungumzia Chelsea
Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte anasema kuwa mkufunzi mwenza katika klabu ya Manchester United Jose Mourinho anafaa kujitazama badala ya kuijadili Chelsea
Conte ameonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu kikosi chake cha Chelsea kufuatia misururu ya majeraha msimu huu na kusema kuwa sare ya 3-3 dhidi ya Roma katika michuano ya vilabu bingwa imekifanya kikosi chake kuwa katika hali ya dharura.
Mourinho ambaye amewahi kuifunza Chelsea mara mbili alinukuliwa akisema kuwa kuna wakufunzi wengine ambao hupenda kulalama sana kuhusu majeraha.
''Kila wakati Mourinho lazima azungumzie kile kinachoendelea Chelsea," alisema Conte
Alipoulizwa kuhusu matamshi ya Mourinho ambayo hayakumlenga Conte moja kwa moja , kocha huyo wa Itali aliongezea: Kila mara , pia msimu uliopita, nadhani ni wakati anafaa kuzungumzia kuhusu kikosi chake na ajitazame badala ya kutazama wenzake

Post Bottom Ad